Your help needed

As we committed ourselves to have our own premises for an improvement and to provide high quality of Islam education for the muslims in Leicester, Madrasatul Noor Leicester would like to take an oppertunity to inform every one who wish to contribute and to support our project to use our account below: Madrassatul Noor Leicester Lloyds TSB Bank Account number: 45127768 Sort Code: 30-94-97 International Bank account: LOYDGB21029 GB27LOYD30949745127768 If you would like to have more information please do not hasitate to contact us through these emails: madrasatulnoor.01@gmail.com or fcalwattan@gmail.com With a lot of thanks

29 Feb 2012

Wimbi la kupinga kuchomwa moto Qur'ani lawafukuza wafanyakazi wa UN Afghanistan



Wimbi kubwa la malalamiko ya wananchi wa Afghanistan dhidi ya kitendo kiovu cha askari wa Marekani cha kuchoma moto Qur'ani Tukufu limewalazimisha wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa kuondoka nchini humo.

Ripoti zinasema Umoja wa Mataifa kama zilivyofanya taasisi nyingine za kimataifa, umelazimika kuwaondoa wafanyakazi wake nchini humo kwa sababu za kiusalama kutokana na machafuko na mapigano yaliyosababishwa na kitendo kiovu cha askari wa Marekani katika kituo cha anga cha Bagram cha kuchoma moto nakala za Qur'ani Tukufu.

Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wameondoka katika mji wa Kunduz huku waandamanaji wakijaribu kuvamia ofisi za taasisi hiyo ya kimataifa.

Maandamano na malalamiko ya wananchi wa Afghanistan dhidi ya kitendo hicho kiovu cha askari wa Marekani yangali yanaendelea licha ya kupita wiki moja tangu askari hao wachome moto nakala za kitabu hicho kitakatifu.

No comments:

Post a Comment