Your help needed

As we committed ourselves to have our own premises for an improvement and to provide high quality of Islam education for the muslims in Leicester, Madrasatul Noor Leicester would like to take an oppertunity to inform every one who wish to contribute and to support our project to use our account below: Madrassatul Noor Leicester Lloyds TSB Bank Account number: 45127768 Sort Code: 30-94-97 International Bank account: LOYDGB21029 GB27LOYD30949745127768 If you would like to have more information please do not hasitate to contact us through these emails: madrasatulnoor.01@gmail.com or fcalwattan@gmail.com With a lot of thanks

25 Sept 2014

Taarifa ya muandamo wa mwezi wa Dhul Hijja, siku ya Arafah na siku ya Eid

As-Salaamu 'Alaykum wa RahmatuLLaah wa Barakaatuh
Tunapenda kuwaatarifu kwamba mwezi wa Dhul-Hijjah umeandama na hivyo siku ya Alkhamis ni mwezi 1 Dhul-Hijjah 1435 (25 Septemba 2014) na ‘Arafah itakuwa ni Siku ya Ijumaa  mwezi 9 Dhul-Hijjah (3 Oktoba 2014) na ‘Eidul-Adhw-haa itakuwa ni Jumamosi mwezi 10 Dhul-Hijjah (4 Oktoba 2014)).
Kadhaalika tunapenda kuwakumbusha ndugu zetu mambo mawili muhimu  tunayoghafilika nayo katika masiku ya Dhul-Hijjah
Kuchinja: Wenye  kunuia kuchinja au kuchinjiwa, wanatakiwa wajizuie kukata nywele na kucha kuanzia unapoingia tu mwezi wa Dhul-Hijjah mpaka watakapomaliza kuchinja. Haya ni maamrisho yanayopatikana katika Hadiyth ifuatayo:
عن أم سلمة رضي الله عنها، أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: (((ِذَا رَأَيْتُمْ هِلَالَ ذِي الْحِجَّةِ وَأَرَادَ أَحَدُكُمْ أَنْ يُضَحِّيَ ، فَلْيُمْسِكْ عَنْ شَعْرِهِ وَأَظْفَارِهِ))) وفي راوية: ((فَلَا يَأْخُذْ مِنْ شَعْرِهِ وَلَا مِنْ أَظْفَارِهِ شَيْئًا ، حَتَّى يُضَحِّيَ)) مسلم
Imetoka kwa Ummu Salamah (Radhiya Allaahu 'anha) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Ukiandama mwezi wa Dhul-Hijjah na ikiwa yuko anayetaka kuchinja basi azuie (asikate) nywele zake na kucha zake) Na katika riwaya nyingine ((Asikate nywele wala kucha mpaka akimaliza kuchinja)) [Muslim na wengineo]
 Source: Alhidaaya

No comments:

Post a Comment