Your help needed

As we committed ourselves to have our own premises for an improvement and to provide high quality of Islam education for the muslims in Leicester, Madrasatul Noor Leicester would like to take an oppertunity to inform every one who wish to contribute and to support our project to use our account below: Madrassatul Noor Leicester Lloyds TSB Bank Account number: 45127768 Sort Code: 30-94-97 International Bank account: LOYDGB21029 GB27LOYD30949745127768 If you would like to have more information please do not hasitate to contact us through these emails: madrasatulnoor.01@gmail.com or fcalwattan@gmail.com With a lot of thanks

13 Mar 2012

Maadui na njama za kukabiliana na Qur'ani na Uislamu


Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt AS amesema kuvunjiwa heshima matukufu ya Kiislamu kupitia vitendo kama vile kuchoma moto Qur'ani ni katika njama za maadui za kukabiliana na Qur'ani Tukufu na Uislamu. Ayatullah Abbas-Ali Akhtari ameongeza kuwa Marekani, utawala wa Kizayuni wa Israel na Uingereza zinatekeleza njama za kuzuia kuenea Uislamu duniani.

Ayatullah Akhtari ameyasema hayo siku ya Jumatano mjini Tehran katika khitma iliyoandaliwa kwa ajili ya watu wa Afghanistan waliouawa shahidi katika maandamano ya kulaani kitendo cha Wamarekani kuchoma moto nakala kadhaa za Qur'ani Tukufu nchini humo hivi karibuni.

Ayatullah Akhtari ameelezea masikitiko yake kuwa wahubiri katika kasri ya mfalme anayejiita kuwa ni Khadimul Haramein wanalinda maslahi ya Marekani na kuunga mkono jinai za dola hilo la kiistikbari.

 Amesema ni jambo la kusikitisha kuona wahubiri hao wakipuuza kitendo cha Wamarekani kuchoma moto Qur'ani na hata hawako tayari kutoa fatwa kuhusu suala hilo.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt AS ameongeza kuwa ni jukumu la kila Muislamu kulaani kitendo cha kuvunjiwa heshima matukufu ya Kiislamu. Ayatullah Akhtari amesema, 'Maadui wafahamu kuwa Waislamu hawatastahamili jinai dhidi ya matukufu ya Kiislamu na kwamba watakabiliana vikali na suala hilo.

No comments:

Post a Comment