Your help needed

As we committed ourselves to have our own premises for an improvement and to provide high quality of Islam education for the muslims in Leicester, Madrasatul Noor Leicester would like to take an oppertunity to inform every one who wish to contribute and to support our project to use our account below: Madrassatul Noor Leicester Lloyds TSB Bank Account number: 45127768 Sort Code: 30-94-97 International Bank account: LOYDGB21029 GB27LOYD30949745127768 If you would like to have more information please do not hasitate to contact us through these emails: madrasatulnoor.01@gmail.com or fcalwattan@gmail.com With a lot of thanks

23 Feb 2012

Picha: 7 wafariki katika maandamano ya kupinga uchomaji Quran moto - Afghanistan


Baadhi ya Quran zilizokutwa zimechomwa moto
Takriban raia saba wa Afghanistan waliuwawa kwa kupigwa risasi na wengine wakajeruhiwa jana katika mapambano kati ya polisi na waandamanaji waliokuwa wakipinga kuchomwa moto Quran, katika kambi moja ya kijeshi ya Marekani.

Mjini Kabul na katika mikoa ya mashariki, kaskazini na kusini mwa mji huo mkuu wananchi wa Afghanistan waliojawa na hasira waliingia mitaani wakipiga kelele zilizosema "Kifo kwa Marekani" huku wakirusha mawe na kuchoma moto maduka na magari, na wakati huohuo milio ya risasi nayo ilisikika.

Katika mji wa mashariki wa Jalalabad, wanafunzi walichoma moto kibonzo cha Rais Barack Obama, huku ubalozi wa Marekani mjini Kabul ukifungwa.

Kamanda wa Marekani nchini Afghanistan, Jenerali John Allen, aliomba radhi kuhusiana na tukio la kuchomwa moto Quran na akaamuru uchunguzi wa kina ufanywe.

Bwana Allen na Naibu Waziri wa Ulinzi wa Marekani Ashton Carter walimwomba msamaha kwa Rais wa Afghanistan Hamid Karzai kwa tukio hilo lililotokea katika kambi ya wanajeshi wa angani iliyopo Bagram. Karzai alimtaka Allen kushirikiana kikamilifu katika uchunguzi wa serikali katika tukio hilo, na akamtaka ahakikishe kuwa matukio ya aina hiyo hayatokei tena.









Raia wa afghanistan wakionyesha kukasirishwa na kitendo cha uchomwaji wa Quran katika kambi moja ya kijeshi ya Marekani huko Afghanistan

Video:

No comments:

Post a Comment