Your help needed

As we committed ourselves to have our own premises for an improvement and to provide high quality of Islam education for the muslims in Leicester, Madrasatul Noor Leicester would like to take an oppertunity to inform every one who wish to contribute and to support our project to use our account below: Madrassatul Noor Leicester Lloyds TSB Bank Account number: 45127768 Sort Code: 30-94-97 International Bank account: LOYDGB21029 GB27LOYD30949745127768 If you would like to have more information please do not hasitate to contact us through these emails: madrasatulnoor.01@gmail.com or fcalwattan@gmail.com With a lot of thanks

15 Feb 2012

Kijana ajichoma moto mbele ya lango la Ikulu Mauritania



Kijana wa Mauritania ambaye bado damu yake inaendelea kuchemka na bado ni nguvu kazi ya Taifa,ameamua kujiwasha moto ili afe mbele ya jengo la Baraza la Seneti la Mauritania karibu na lango kuu la Ikulu ya Rais katikati ya mji mkuu wa Mauritani, Nouakchott-jioni ya siku ya Alhamisi.
Walinzi wa Ikulu ya Rais, waliingilia kati na kuanza kuuzima moto na kumkimbiza Hospitalini,akiwa bado yuko hai.


Mpaka sasa haijulikana afya ya kijana huyu huko Hospitalini na hata sababu iliyopelekea kijana huyu ajichome moto bado haijajulikana.Ispokuwa baadhi ya vyanzo vya habari vimesema kwamba:

Kijana huyu ni mmoja kati ya wale waliobeba vyeti vya wasiokuwa na kazi au wasiokuwa na ajira na ambao walitishia hapo mwanzo kuwa ikiwa hawatozingatiwa na kupata ajira basi watajichoma moto wenyewe,na hii ilikuwa ni baada ya kuvichoma moto vyeti vyao vya kielimu kutokana na kukata tamaa.

Tukio hili ni la aina yake kutokea nchini Mauritania tangu kijana mwingine aliyeitwa Yaqub mtoto wa Dahud kujichoma moto mwenyewe mwaka uliopita katika sehemu hiyo hiyo alipokijana huyu akiungua moto kama anavyoonekana kwenye picha.

No comments:

Post a Comment