Your help needed

As we committed ourselves to have our own premises for an improvement and to provide high quality of Islam education for the muslims in Leicester, Madrasatul Noor Leicester would like to take an oppertunity to inform every one who wish to contribute and to support our project to use our account below: Madrassatul Noor Leicester Lloyds TSB Bank Account number: 45127768 Sort Code: 30-94-97 International Bank account: LOYDGB21029 GB27LOYD30949745127768 If you would like to have more information please do not hasitate to contact us through these emails: madrasatulnoor.01@gmail.com or fcalwattan@gmail.com With a lot of thanks

25 Sept 2014

Tangazo la Sala ya Eid Al Hajj Leicester


Asalaam aleykum, An Noor Community Centre wakishirikiana na Madrasatul Noor Leicester wanawajulisha waislamu wote ya kuwa panapo majaaliwa sala Eid Al Hajj itasaliwa siku ya Jumamosi tarehe 4 October 2014 hapo katika msikiti wa An Noor Leicester. Takbeer zitaanza saa mbili na robo asububuhi (08.15 am) na sala itasaliwa saa mbili na nusu (08.30 am).

Kama kawaida wanaume watakuwa eneo la chini na wanawake wao watakuwa eneo la juu. Tafadhali jitahidi kufika mapema.
Shukran

Taarifa ya muandamo wa mwezi wa Dhul Hijja, siku ya Arafah na siku ya Eid

As-Salaamu 'Alaykum wa RahmatuLLaah wa Barakaatuh
Tunapenda kuwaatarifu kwamba mwezi wa Dhul-Hijjah umeandama na hivyo siku ya Alkhamis ni mwezi 1 Dhul-Hijjah 1435 (25 Septemba 2014) na ‘Arafah itakuwa ni Siku ya Ijumaa  mwezi 9 Dhul-Hijjah (3 Oktoba 2014) na ‘Eidul-Adhw-haa itakuwa ni Jumamosi mwezi 10 Dhul-Hijjah (4 Oktoba 2014)).
Kadhaalika tunapenda kuwakumbusha ndugu zetu mambo mawili muhimu  tunayoghafilika nayo katika masiku ya Dhul-Hijjah
Kuchinja: Wenye  kunuia kuchinja au kuchinjiwa, wanatakiwa wajizuie kukata nywele na kucha kuanzia unapoingia tu mwezi wa Dhul-Hijjah mpaka watakapomaliza kuchinja. Haya ni maamrisho yanayopatikana katika Hadiyth ifuatayo:
عن أم سلمة رضي الله عنها، أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: (((ِذَا رَأَيْتُمْ هِلَالَ ذِي الْحِجَّةِ وَأَرَادَ أَحَدُكُمْ أَنْ يُضَحِّيَ ، فَلْيُمْسِكْ عَنْ شَعْرِهِ وَأَظْفَارِهِ))) وفي راوية: ((فَلَا يَأْخُذْ مِنْ شَعْرِهِ وَلَا مِنْ أَظْفَارِهِ شَيْئًا ، حَتَّى يُضَحِّيَ)) مسلم
Imetoka kwa Ummu Salamah (Radhiya Allaahu 'anha) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Ukiandama mwezi wa Dhul-Hijjah na ikiwa yuko anayetaka kuchinja basi azuie (asikate) nywele zake na kucha zake) Na katika riwaya nyingine ((Asikate nywele wala kucha mpaka akimaliza kuchinja)) [Muslim na wengineo]
 Source: Alhidaaya

11 Sept 2014

Documentary: British women are converting to Islam


Tangazo la Muhadhara Leicester Uingereza



Asalaam Aleykum,

Ndugu zangu katika IMANI, An Noor Community Centre wakishirikiana na Madrassatul Noor Leicester kwa pamoja wanakualika muhadhara wa dini ya kiislamu utakaofanyika siku ya Jumamosi ya tarehe 27/09/2014, katika msikiti wa An Noor kuanzia saa kumi kamili jioni (4pm).

Muhadhir mkuu atakuwa Sheikh Nassor kutoka London.

Waislamu wote wa kike na wa kiume wanakaribishwa. Wanawake nafasi yao itakuwa eneo la juu ya msikiti.

Tafadhali jitahidi kuisambaza habari hii ya muhadhara kwa waislamu wengine.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na:
Abdul Dau: 07792104495
Ustadh Farid: 07792174408
Ustadh Issa: 07984106983

Anuani kamili ya msikiti ni:
170a Belgrave Gate
Leicester
LE1 3XL

Wabillah Tawfiq