Your help needed

As we committed ourselves to have our own premises for an improvement and to provide high quality of Islam education for the muslims in Leicester, Madrasatul Noor Leicester would like to take an oppertunity to inform every one who wish to contribute and to support our project to use our account below: Madrassatul Noor Leicester Lloyds TSB Bank Account number: 45127768 Sort Code: 30-94-97 International Bank account: LOYDGB21029 GB27LOYD30949745127768 If you would like to have more information please do not hasitate to contact us through these emails: madrasatulnoor.01@gmail.com or fcalwattan@gmail.com With a lot of thanks

29 Feb 2012

Wimbi la kupinga kuchomwa moto Qur'ani lawafukuza wafanyakazi wa UN Afghanistan



Wimbi kubwa la malalamiko ya wananchi wa Afghanistan dhidi ya kitendo kiovu cha askari wa Marekani cha kuchoma moto Qur'ani Tukufu limewalazimisha wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa kuondoka nchini humo.

Ripoti zinasema Umoja wa Mataifa kama zilivyofanya taasisi nyingine za kimataifa, umelazimika kuwaondoa wafanyakazi wake nchini humo kwa sababu za kiusalama kutokana na machafuko na mapigano yaliyosababishwa na kitendo kiovu cha askari wa Marekani katika kituo cha anga cha Bagram cha kuchoma moto nakala za Qur'ani Tukufu.

Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wameondoka katika mji wa Kunduz huku waandamanaji wakijaribu kuvamia ofisi za taasisi hiyo ya kimataifa.

Maandamano na malalamiko ya wananchi wa Afghanistan dhidi ya kitendo hicho kiovu cha askari wa Marekani yangali yanaendelea licha ya kupita wiki moja tangu askari hao wachome moto nakala za kitabu hicho kitakatifu.

Injili ya kale iliyogunduliwa nchini Uturuki yaonesha utabiri wa kudhihiri Mtume Muhammad SAW



Nakala ya Injili ya miaka 1500 iliyopita na ambayo imepatikana tena katika kanisa moja nchini Uturuki baada ya kupotea kwa muda wa miaka 12, ina utabiri wa kuja Mtume wa Uislamu, Nabii Muhammad SAW baada ya Masihi Issa yaani Yesu AS.

Vyombo vya habari vimeripoti kuwa, nakala hiyo ya zamani sana ya Injili imeandikwa kwa lugha ya Kiarami na vyombo vya habari vinasema kuwa, ilikuwa imefichwa kwa muda wa miaka 12.

Tayari viongozi wa Vatican wameonesha hamu kubwa ya kuipata Injili hiyo na Papa Benedict wa 16 ametoa mwito wa kufanyiwa uchunguzi maandishi ya Injili hiyo.

Kwa upande wake, Waziri wa Utamaduni wa Uturuki, Ertuğrul Günay amesema kuwa, bei ya Injili hiyo ni dola milioni 22 za Kimarekani na kwa vile utabiri wa kuja Mtume Muhammad SAW unapatikana kwenye Injili hiyo yenye lugha ya Nabii Issa AS, ilikuwa imefichwa ili watu wasiione.

Amesema maneno yaliyomo kwenye Injili hiyo ya miaka 1500 iliyopita yanafanana sana na maneno ya Qur'ani Tukufu na kiujumla maneno yake yanakaribiana sana na mafundisho ya Uislamu.

Sehemu moja ya maneno yaliyomo kwenye Injili hiyo yanamtaja Yesu kuwa ni mwanadamu na kumnukuu Nabii huyo wa Mwenyezi Mungu akisema kuwa, Mtume atakayekuja baada yake anaitwa Muhammad. Sehemu ya maneno ya Injili hiyo ya miaka 1500 iliyopita yana maana isemayo: Kuhani mmoja alimuuliza Masihi Yesu kuhusu mtu atakayekuja kuchukua nafasi yake na Yesu akajibu: "Muhammad (SAW) ndilo jina lake lililobarikiwa, anatoka katika kizazi cha Ismail, baba yangu Mwarabu."

Waziri wa Utamaduni wa Uturuki pia amesema, tayari Papa Benedict wa 16 ametuma maombi rasmi ya kutaka wapatiwe Injili hiyo iliyopatikana kwenye visiwa vya Uturuki vilivyoko kwenye bahari ya Mediterranean. Imeelezwa kuwa watu waliopatikana na Injili hiyo walikuwa wana nia ya kuiuza kimagendo na hivi sasa wanashikiliwa katika mahakama za Uturuki.

Wakati huo huo kasisi Ihsan Uzbek, mmoja wa viongozi waandamizi wa Kikristo nchini Urutuki amesema kuwa Injili hiyo ni ya zama za mtakatifu Barnaba aliyeishi na Nabii Issa na ambaye alikuwa mfuasi wake wa karibu.

Huko nchini Uturuki nako kumetolewa mwito wa kufanyika uchunguzi wa kitaalamu wa kuweza kujua tarehe hasa ilipoandikwa Injili hiyo.

26 Feb 2012

Nimeipenda hii


Msikiti Madina

Picha: Maulidi ya mfungo sita Toronto Canada

Khalfan Abdullah Katika mpango mzima kusoma maulidi ya Mfungo Sita ya Mtume Muhammad. (S.A W) Yaliosomwa siku ya jumamosi Feb 18,2012 katika ukumbi wa lawrence heights commnity centre
Canada Toronto.

Baadhi ya wanafunzi wa Madrasatul Al-Amin akisoma maulidi ya Mfungo Sita ya Mtume Muhammad. (S.A .W)

Wanafunzi wa Madrasatul Al-Amin Nchini Canada Toronto akisoma maulidi ya Mfungo Sita ya Mtume Muhammad. (S.A W)

Wazee wamoja na wanafunzi wa kike wakiwa kwenye Mfungo Sita ya Mtume Muhammad. (S.A W) yaliosomwa siku ya Jumamosi Feb 18, 2012

Ustadhi Abdalluh Abukakar Mtawa akitoa mawili matatu kwenye sherehe hizo za maulidi ya Mtume wetu Muhammad. (S.A W) yanayofanyika kila mwaka ifikapo mwenzi wa kiislamu mfunga sita.

Ustadhi Jamal (kulia) akishirikiana na wanafunzi wa Madrasatul Al-Amin kwenye akisoma cha maulidi ya Mfungo Sita ya Mtume Muhammad. (S.A .W)

Mashaallah wakina mama nao walishiriki kikamilifu

Saving Somalia: A wasted effort?

23 Feb 2012

Urusi yawaonya Israel juu ya Iran


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Gennadi Gatilov

Urusi kwa mara nyingine imeuonya utawala haramu wa Israel kuhusu maafa makubwa yatakayojiri iwapo utawala huo utathubutu kuishambulia kijeshi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Gennadi Gatilov amesema mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Iran yatasababisha maafa makubwa kieneo na kimataifa.

Marekani, utawala wa Kizayuni wa Israel na waitifaki wao wamekuwa wakiituhumu Iran kuwa ina malengo ya kijeshi katika mpango wake wa nyukla. Kwa kisingizio hicho wamekuwa wakitoa vitisho vya kuishambulia Iran kijeshi.
Iran inasisitiza kuwa shughuli zake za nyuklia zinafanyika kwa malengo ya amani. Aidha Iran inasema kwa vile ni mwanachama wa Mkataba wa Kuzuia Utengenezaji na Usambazaji Silaha za Nyuklia NPT na vile vile kama mwanachama wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA ina haki ya kutumia teknolojia ya nyuklia kwa malengo ya amani.

Balozi Seif afungua jengo la Madrasa Hidayatul Islamiyah


Makamu wa pili wa Rais akikagua moja ya jeongo la Madrasa Hidayatul Islamia

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema ipo haja kwa Washirika na Wafadhili wa Maendeleo katika nyanja za Elimu ya Dini ndani na nje ya Nchi kufikiria zaidi wazo la kuongeza nguvu katika ujenzi wa Vyuo na Madrasa ili kuwajengea mazingira bora ya Kitaaluma watoto wa Taifa hili.

Kauli hiyo ameitoa mara baada ya kulifunguwa Jengo Jipya la Madrasa Hidayatul Islamia iliyopo Njia Kuu Moga ndani ya Wadi ya Gamba Wilaya ya Kaskazini A.

Balozi Seif alisema Jamii ya Kiislamu imeshuhudia ongezeko kubwa la Ujenzi wa Misikiti Nchini kasi ambayo inaweza pia kuelekezwa katika Vyuo na Madrasa ambayo Maeneo mengi yamekuwa na ufinyu wa Majengo hao ya Kudumu.

“ Sisemi kwamba Wafadhili wasijenge Misikiti la hasha. Lakini ni vyema kwa wafadhili wakaangalia mazingira ya Vyuo na Madrasa nyingi Nchini ambazo ama ni mbovu au hazina hadhi ya kusomeshea kitabu cha Mwenyezi Muungu ”. Alishauri na Kusisitiza Balozi Seif.

Makamu wa Pili wa Rais waZanzibaralimpongeza Mfadhili wa Madrasda hiyo Ukti Asia Mohd wa Oman kwa juhudi zake za kusaidia kupanua Elimu ya Dini Hapa Nchini.

“ Nimevutiwa na Madrasa hii. Nilipoikagua ndani nimeona Darasa la Watu Wazima. Hii ni ishara na fursa nzuri kwa nao kupata wasaa wa kujielimisha. Kwa kweli Madrasa zina umuhimu wa kipekee katika kutanua Elimu popote pale ”. Alifafanua Balozi Seif.

Balozi Seif aliwataka Vijana kuhakikisha wanaitafuta Elimu kwa Njia yoyote huku akiisisitiza Jumuiya inayosimamia masuala ya Elimu ya Dini Wilaya ya Kaskazini “A” { JUVMAWA } ikaendelea kuonyesha Njia bora kwa Watoto wanaowalea.


Balozi Iddi akimkabidhi mmoja ya wanfunzi kitabu

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ameahidi kutoa Mchango wa Kompyuta moja kwa ajili ya Madrasa hiyo na kuutaka Uongozi wa Jimbo la Chaani, Wilaya ya Kaskazini A na Mkoa wa Kaskazini kuhakikisha changamoto zinazoikabili Madrasa hiyo zinatatuliwa.

Katika Risala ya Madrasa hiyo iliyosomwa na Ustadhi Khamis Hakim alisema Madrasa hiyo iliyoasisiwa zaidi ya miaka 80 ikiwa na Wanafunzi 500 mchanganyiko imekuwa chemchem ya kutoa walimu wanaoendelea kusomesha Madrasa tofauti Wilayani humo.

Wakati huo huo mamia ya Waumini wa Dini ya Kiislamu na Wananchi wamehudhuria Maulidi ya Uzawa wa Kiongozi wa Dini ya Kiislamu Mtume Muhammad { SAW }.

Maulidi hayo yaliandaliwa na Uongozi wa Masjid Noor Muhammad{ SAW } iliyopo Mtaa waMombasakwaChinaambapo Makamu wa Pili wa Rais waZanzibarBalozi Seif alikuwa Mgeni Rasmi kwenye Hafla hiyo.

Akitoa chakula cha moyo katika hadhara hiyo Mwanachuoni Maarufu ndani ya Mwambao waTanzaniaSheikh Sameer Zulfikar amewaasa Waumini wa Dini ya Kiislamu kutouacha Mwezi huu ukapita bila ya kusafisa nyoyo zao kwa kumtukuza Mtume Muhammad { SAW }.

Suratul- Fatha

بسم الله الرحمن الرحيم(1) 

الْحَمْدُ للّهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ (2) الرَّحْمـنِ الرَّحِيمِ (3) مَالِكِ يَوْمِ الدِّينِ (4) إِيَّاكَ نَعْبُدُ وإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ (5) اهدِنَــــا الصِّرَاطَ المُستَقِيمَ (6)

صِرَاطَ الَّذِينَ أَنعَمتَ عَلَيهِمْ غَيرِ المَغضُوبِ عَلَيهِمْ وَلاَ الضَّالِّينَ (7)

Picha: 7 wafariki katika maandamano ya kupinga uchomaji Quran moto - Afghanistan


Baadhi ya Quran zilizokutwa zimechomwa moto
Takriban raia saba wa Afghanistan waliuwawa kwa kupigwa risasi na wengine wakajeruhiwa jana katika mapambano kati ya polisi na waandamanaji waliokuwa wakipinga kuchomwa moto Quran, katika kambi moja ya kijeshi ya Marekani.

Mjini Kabul na katika mikoa ya mashariki, kaskazini na kusini mwa mji huo mkuu wananchi wa Afghanistan waliojawa na hasira waliingia mitaani wakipiga kelele zilizosema "Kifo kwa Marekani" huku wakirusha mawe na kuchoma moto maduka na magari, na wakati huohuo milio ya risasi nayo ilisikika.

Katika mji wa mashariki wa Jalalabad, wanafunzi walichoma moto kibonzo cha Rais Barack Obama, huku ubalozi wa Marekani mjini Kabul ukifungwa.

Kamanda wa Marekani nchini Afghanistan, Jenerali John Allen, aliomba radhi kuhusiana na tukio la kuchomwa moto Quran na akaamuru uchunguzi wa kina ufanywe.

Bwana Allen na Naibu Waziri wa Ulinzi wa Marekani Ashton Carter walimwomba msamaha kwa Rais wa Afghanistan Hamid Karzai kwa tukio hilo lililotokea katika kambi ya wanajeshi wa angani iliyopo Bagram. Karzai alimtaka Allen kushirikiana kikamilifu katika uchunguzi wa serikali katika tukio hilo, na akamtaka ahakikishe kuwa matukio ya aina hiyo hayatokei tena.









Raia wa afghanistan wakionyesha kukasirishwa na kitendo cha uchomwaji wa Quran katika kambi moja ya kijeshi ya Marekani huko Afghanistan

Video:

15 Feb 2012

Kijana ajichoma moto mbele ya lango la Ikulu Mauritania



Kijana wa Mauritania ambaye bado damu yake inaendelea kuchemka na bado ni nguvu kazi ya Taifa,ameamua kujiwasha moto ili afe mbele ya jengo la Baraza la Seneti la Mauritania karibu na lango kuu la Ikulu ya Rais katikati ya mji mkuu wa Mauritani, Nouakchott-jioni ya siku ya Alhamisi.
Walinzi wa Ikulu ya Rais, waliingilia kati na kuanza kuuzima moto na kumkimbiza Hospitalini,akiwa bado yuko hai.


Mpaka sasa haijulikana afya ya kijana huyu huko Hospitalini na hata sababu iliyopelekea kijana huyu ajichome moto bado haijajulikana.Ispokuwa baadhi ya vyanzo vya habari vimesema kwamba:

Kijana huyu ni mmoja kati ya wale waliobeba vyeti vya wasiokuwa na kazi au wasiokuwa na ajira na ambao walitishia hapo mwanzo kuwa ikiwa hawatozingatiwa na kupata ajira basi watajichoma moto wenyewe,na hii ilikuwa ni baada ya kuvichoma moto vyeti vyao vya kielimu kutokana na kukata tamaa.

Tukio hili ni la aina yake kutokea nchini Mauritania tangu kijana mwingine aliyeitwa Yaqub mtoto wa Dahud kujichoma moto mwenyewe mwaka uliopita katika sehemu hiyo hiyo alipokijana huyu akiungua moto kama anavyoonekana kwenye picha.

Mtoto wa kiswahili awashangaza watangazaji wa TV kwa kipaji chake

4 Feb 2012

An Noor Muslim Community Centre Leicester Project Appeal








Madrasatul Noor is an Islamic school established in 1999 with few Swahili speakers parents from East Africa living in Leicester.

At the beginning we started with few students where we used to use one of our teacher's resident.

But because of the increased number of the students, in 2003 our community has decided to rent a building for the purpose of providing high quality of education.

Alhamdulillah, our Madrasah has been developing and progressing in very high pace. So now the space on our current building has become very limited.

In 2010 we have decided to find our own premises. Alhamdulillah we have manage to find one building which is going to be very perfect for our needs.

The building has got enough spaces for the mosque, classes, Library and conference room.

As we committed ourselves to have our own premises for an improvement and to provide high quality of Islam education for the muslims in Leicester, Madrasatul Noor Leicester would like to take an oppertunity to inform every one who wish to contribute and to support our project to use our account below:

Madrassatul Noor Leicester
Lloyds TSB Bank

Account number: 45127768

Sort Code: 30-94-97

International Bank account:

LOYDGB21029


GB27LOYD30949745127768

If you would like to have more information please do not hasitate to contact us through these emails:

madrasatulnoor.01@gmail.com
or
fcalwattan@gmail.com


With a lot of thanks